Na Francis Godwin,Iringa
MTAMBUE kijana Frank Joseph Kalenga (37) mkazi wa Mtaa wa Ngelewala Kata ya Mwangata mjini Iringa aliyepata kuwa mfanyabiashara mkubwa. Kwa sasa amegeuka omba omba katika mji wa Iringa baada ya kucharangwa mapanga usoni na kupata ulemavu macho (upofu ) wa kudumu.