Featured, Habari, Headline, Jamii »

[2 Jan 2013 | Comments Off | 93 views]
Mwandishi wa Channel Ten ashambuliwa

Na Burhani Yakub, Tanga
MWANDISHI wa habari wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten Tanga, Linus Kamafa amejeruhiwa vibaya na vijana waliokuwa wakichoma matairi na kulipua baruti wakati wakisherehekea mkesha wa Mwaka Mpya.
Vijana hao wanadaiwa kumshambulia kwa mawe na mapanga mwandishi huyo wa habari wakidhani ni miongoni mwa askari  Polisi waliokuwa wakipita mitaani kuzuia uchomaji moto wa matairi na kulipua baruti.
Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga,Constantine Massawe ni kuwa mwandishi huyo wa habari alishambuliwa juzi saa 6.30 usiku katika Mtaa wa Mapinduzi jijini …

Featured, Habari, Headline, Jamii, Siasa »

[2 Jan 2013 | Comments Off | 126 views]
Rais awashukia viongozi wa dini, wanasiasa

Na Florence Majani
RAIS Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa dini na wanasiasa kupima kauli na vitendo vyao ili kuepusha kuligawa taifa kwa misingi ya imani za dini na itikadi za siasa, kama ilivyotaka kujitokeza mwaka 2012.
Katika salamu zake za Mwaka Mpya kwa Taifa juzi, Rais Kikwete alisema kwa mara ya kwanza mwaka  2012, Tanzania ilifikishwa kwenye hatari ya kutokea mgawanyiko wa Watanzania au hata mapigano kwa misingi ya dini zao.
“Nimeshalisemea jambo hili siku za nyuma na napenda kurudia leo kuwasihi Watanzania wenzangu kupima athari za kauli zetu na matendo yetu kwa mustakabali …

Featured, Habari, Headline, Jamii »

[2 Jan 2013 | Comments Off | 104 views]
Mbunge wa CCM ampinga JK gesi kwenda Dar

MBUNGE wa Mtwara Mjini (CCM), Hasnain Murji na Mwenyekiti wa CCM Manispaa ya Mikindani, Ali Chinkawene wamepinga kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwamba wakazi wa Mkoa wa Mtwara hawapaswi kuzuia gesi kwenda Dar es Salaam.
Juzi, katika salamu zake za Mwaka Mpya, Rais Kikwete alipinga madai ya wakazi wa Mikoa ya Kusini kutaka gesi hiyo isisafirishwe kwenda Dar es Salaam, akisema madai hayo hayakubaliki popote.
“Rasilimali inayopatikana popote katika nchi hii ni mali ya taifa zima na hutumika kwa manufaa ya taifa na katu si mali ya watu wa pale ilipogundulika au …

Featured, Habari, Headline, Jamii, Siasa, Uchunguzi »

[2 Jan 2013 | Comments Off | 125 views]
From Dar to Goma: How I met, and had lunch with rebels

By Richard Mgamba
30th December 2012
It was seven days before Christmas eve, the period in which Christians all over the world are busy with shopping and planning for the celebration of the birth of Jesus Christ, but to me it was a scary and memorable day — the day I chatted and lunched with M23 rebels’ top commander, General Sultan Emanuel Makenga, a 39-year-old soldier, who has fought three different wars in three different countries of Uganda, Rwanda and Congo, but still willing to fight till his last blood.
It was frightening …

Featured, Habari, Headline, Jamii »

[26 Dec 2012 | Comments Off | 167 views]
Tas Mwanza yalaani albino kuzikwa ndani ya duka

(ErnestKimaya mwenyekiti wa Tas Taifa)
Na George Ramadhan
26th December 2012
Chama  cha Watu Wenye Ulemavu wa Ngozi (Tas) mkoani Mwanza, kimelaani vikali kitendo cha familia moja wilayani Magu kumzika ndani ya chumba cha biashara mtoto wao mwenye ulemavu wa ngozi (albino).
Mtoto huyo aliaga dunia Desemba 15, mwaka huu nyumbani kwao mjini Magu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Tas Mkoa wa