Home » Mjengwablog

Mjengwablog


One Comment »

  • Joseph Mbele said:

    Mheshimiwa Mwenyekiti

    Ninayo habari ambayo imenigusa sana. Niko huku Marekani. Jana nilipigiwa simu na mdogo wangu aliyeko kijijini kwetu, milimani juu kule Umatengo, Wilaya ya Mbinga, Mkoani Ruvuma. Anasema kuwa amepewa nakala ya “Kwanza Jamii” ambayo ina makala yangu ya “Maendeleo ni Nini?” Inaonekana mhusika alinunua gazeti hili mjini Mbinga, au labda Songea.

    Mdogo wangu ameniambia kuwa watu pale kijijini wamefurahi sana kusoma makala hii na wanaizungumzia sana. Ananiambia ni muhimu niendelee kuandika, maana wote wanataka hivyo.

    Nimefurahi sana kuwa Mheshimiwa Mwenyekiti ulinishauri niwe naandika katika hili gazeti la “Kwanza Jamii.” Hayo ninayoyasikia kutoka kijijini kwangu yamenipa changamoto kubwa.

    Halafu, mdogo wangu amekumbushia mazungumzo ambayo niliwahi kuwa na wanakijiji miaka kadhaa iliyopita, kuhusu vitabu. Nilikuwa nimetamka kuwa ningewapelekea vitabu. Sasa, kutokana na msisimko wa makala yangu katika “Kwanza Jamii,” wanakijiji wanataka nipeleke vitabu.

    Ndio kusema, “Kwanza Jamii” imeleta ari ya usomaji kwa namna ya pekee pale kijijini kwangu. Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona nikueleze hivyo, utambue ni jinsi gani “Kwanza Jamii” inavyoweza kuingia kijijini na kuchangia mabadiliko. Naahidi kuendelea kuandika makala katika “Kwanza Jamii.”

    Wasalaam

    Joseph L. Mbele
    http://www.hapakwetu.blogspot.com