Ni ziara ya kichama. Leo atahitisha sherehe za miaka 33 ya CCM kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.
Read the full story »Serikali imekiri kuwa mpaka kati ya Tanzania na Malawi ni suala lenye utata unaosababisha mvutano unaohitaji ufumbuzi wa haraka.
Kukiri huko kulifanywa jana bungeni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alipokuwa akijibu maswali ya papo kwa papo.
“Anachosema mbunge ni kweli kwamba kumekuwa na mvutano au ubishi kati ya upande wa Malawi na sisi juu kuhusu mpaka hasa uko wapi, ni kati au pembeni mwa ziwa au pembeni mwa Tanzania,” alisema Pinda.
Na Mwandishi Maalum
5/2/2010
New York
Juhudi za nchi zinazoendelea za kuutokomeza umaskini na upatikaji wa ajira zenye hadhi na tija, hazitaweza kufanikiwa kama wananchi maskini na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi, hawatashirikishwa katika utoaji na upitishaji wa maamuzi yanayohusu mustakabali wao.
Mbunge wa Mufindi, Joseph Mungai jana aliibua tena mjadala wa ukomo wa vipindi vya ubunge na viti maalum akieleza kuwa wanaozungumzia suala hilo, wanakwenda kinyume cha katiba inayokataza aina yoyote ya ubaguzi.
Mungai mmoja wa wabunge wenye umri mkubwa na muda mrefu katika bunge hilo, alitoa kauli hiyo juzi bungeni mjini Dodoma wakati akichangia azimio la bunge kuridhia itifaki ya jinsia na Maendeleo ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ya mwaka 2008.